๐บ๐บ๐บ๐บ๐บ๐บ๐บ๐บ๐บ๐บ๐บ๐บ๐บ๐บ๐บ๐บ๐บ๐บ๐บ๐บ๐บ๐บ๐บ๐บ๐บ๐บ๐บ๐บ๐บ๐บ๐บ๐บ๐บ๐บ๐บ๐บ๐บ๐บ๐บ๐บ๐บ๐บ๐บ๐บ
MKRISTO AMKA USINGIZINI SASA!!!!!
MKRISTO AMKA USINGIZINI SASA!!!!!
⏩⏩⏩⏩Ahsante Ee Yesu Kristo Kwa NEEMA yako juu ya kila ambaye ni Mkristo anayesoma chapisho hili. Ee Baba Mungu mjazie neema ya kudumu katika pendo lako na kuyatenda yale yote yaliyo mapenzi yako. Ni kweli kwamba kuna wengine wengi ambao bado hawajakata shauri la kumpokea Yesu Kristo kuwa Bwana na mwokozi wa maisha yao lakini kupitia wapendwa hawa wachache; maisha yao yakawe mfano kwa wengine yakawe na ushawishi juu ya wengine ili wamkubali Yesu Kristo. Amen.⏪⏪⏪⏪⏪⏪⏪
⏬⏬⏬⏬⏬⏬⏬⏬⏬⏬⏬⏬⏬⏬⏬⏬⏬⏬⏬⏬⏬⏬⏬⏬⏬⏬⏬⏬⏬⏬⏬⏬⏬⏬⏬⏬⏬⏬⏬⏬⏬⏬⏬⏬⏬⏬⏬⏬⏬⏬⏬⏬⏬⏬⏬⏬⏬
➤Mpendwa msomaji nakusalimu Katika jina La Bwana wetu Yesu Kristo!
Ni hakika kwamba asilimia kubwa ya WAKRISTO katika karne hii ni wakristo kwa kuzaliwa japo kuna wachache ambao ni wakristo kwa kukata shauri walikuwa sio wakristo lakini wamekubali kubatizwa na kuwa Wakristo. na ndio kusudi la Yesu Kristo la kuujia ulimwengu. alifanyika mwili na akakaa kwetu na alikubali kuteswa na kufa kwaajili ya ulimwengu wote ili kila aliyepotea apate wokovu. alisema mwenyewe kwamba amekuja kwaajili ya kile kilichopotea. amekuja kwaaajili ya yule asiyeokoka, hivyo ni furaha kuu mbinguni mwenye dhambi mmoja anapookoka. ni shangwe na furaha tele, pia ni huzuni kwa mwenye dhambi anapofariki.
➻Ni jukumu lako wewe unayemcha Mungu kuishi maisha yanayompendeza Mungu na yenye mfano kwa wengine. KILA MKRISTO NI MHUBIRI, tuna mhubiri Kristo kupitia matendo yetu. matendo yetu yanamchango wa zaidi ya asilimia 60 katika kkumbadilisha mtu wa imani nyingine. Mf. TUKIISHI MAISHA YA UPENDO- maisha ya upendo ni moja ya maisha ambayo mristo wa aina yeyote ile anapaswa kuyaishi. Ni kweli kwamba majirani aua rafiki yako anaweza kukukosea lakini kumbuka kwamba MUNGU tunaye mwamini na kumtegemea ni PENDO, yeye hakuhesabu maovu yetu tulimkosea sana, tulimkana lakini alituhurumia hata akamtoa mwanaye mpendwa afe kwaajili ya dhambi zetu.
➻Katika sehemu nyengine ya Biblia Yesu Kristo anatuita rafiki zake. Haijalishi ni uovu wa namna gani jirani yako amekutendea lakini unapaswa kumsamehe na kumtendea wema. Neno la Mungu linatuambia kwamba, Jirani yako akikukosea msamehe. lakini linatuambia kwamba mtendee wema jirani yako kwasababu unapofanya hivyo basi unampalia makaa ya mawe juu ya kichwa chake. kumpalia makaa ya mawe juu ya kichwa chake kuna maana hii: unampa uchungu na majuto juu ya kile kitendo ambacho amekutendea.
➻Maisha ya Mkristo yanapaswa yamzalie Mungu matunda. MUNGU hutupa mafanikio na maisha bora ili katika vitu vyote tumzalie matunda. Yohana (sura ya 15) anatuambia kwamba, Yesu Kristo amejiita yeye kama Mzabibu na sisi ni matawi, na kila tawi lisilo zaa basi Mungu ambaye ndiye mkulima basi hulikata. Ili Mungu afurahie maisha yako naakuzidishe katika kila unachokifanya basi unapaswa umzalie matunda. MATUNDA ANAYOHITAJI MUNGU, ni pamoja na wengine wasio mjua Mungu wamjfahamu kupitia wewe; kunena kwako , kutembea kwako hata maamuzi yako.
➻Kwa mali zako na akili pia vyote Mungu alivyokupa unapaswa umtumikie. Yesu Kristo anasema mwenye kanzu mbili umpe asiye nayo. pia mtu mhitaji anapokuja kwako akiwa na uhitaji umkopeshe au umpe basi kama unacho umpe usimwambie aende alafu arudi kesho. zidisha upendo wako kwa kila mmoja lia na anayelia, furahi na anayefurahi huo ndio upendo wa kweli na maisha ya Kikristo. kupitia kufanya hivyo basi utamshawishi yule aliyemtenda dhambi aokoke na kuiacha njia yake mbaya na utapata thawabu mbinguni.
➻Wewe uliye mhubiri huwezi kumhubiria mtu aache dhambi alafu wewe mwenyewe unatenda. kuwa wakwanza kuchukia uovu na kuuacha kabisa na hapo ata ukimwambia mwenye dhambi aache dhambi basi atakubali. pia msaidie kimwili pia usimwache ateseke hana chakula wakati wewe unacho. msaidie kwa kadri ya uwezo Mungu aliokujalia.
NB: Mkristo uliozaliwa katika ukristo, jiulize swali hili; kwanini yule asiye mkristo akiokoka anakuwa na bidiii sana ya kumtafuta Mungu na kiwango chake cha imani kinakuwa sana?
MUNGU AKUBARIKI KWA KUSOMA CHAPISHO HILI!!!!!!!
SHARE CHAPISHO HILI KWA WAKRISTO WENGI UWEZAVYO ILI MKRISTO AAMKE SASA NA KUJITAMBUA.
soma zaidi kwenye ukurasa huu.
christiansforum1.blogspot.com
pokeaeli.blogspot.com
facebook. Joyful house in Jesus Christ
WhatsApp: 0752513159
Maisha yangu Maajabu yanashangaza ushuhuda, Jinsi nimepata kisanduku chenye nguvu sana ambacho sasa ni pesa yangu mara mbili kutoka mia hadi elfu ya pesa ndani ya masaa 24, na pia jinsi nimerudisha mpenzi wangu wa zamani, sababu kuu niliwasiliana na Dk Lomi kwa msaada mimi kumrudisha mpenzi wangu wa zamani, basi ananisaidia ni nguvu kubwa ya kumrudisha mpenzi wangu wa zamani, na ananipenda na ananithamini sasa, basi mimi na Dr Lomi tukawa marafiki, baada ya mazungumzo kadhaa namuuliza ikiwa kuna njia anaweza kuniganga ili nipate pesa, hapo ndipo aliponiambia juu ya sanduku hili la uchawi, akaniambia kuna aina na saizi tofauti ya sanduku, aliniambia aina zote za sanduku, ningeweza kumudu ndogo tu ya sanduku, baada ya maombi muhimu anayofanya kwenye sanduku, ananipeleka kupitia huduma ya kujifungua, aliniambia niweke pesa ndani, niliweka ndani ya sanduku 100 euro baada ya masaa 24 nikagundua ilikuwa elfu 10 euro ndani, na nimekuwa nikitumia sanduku kwa miezi 7 sasa, mimi na mchumba wangu tunaishi maisha bora, ikiwa unahitaji b ack mpenzi wako au pesa spell wasiliana na Dr Lomi kwa barua pepe: lomiultimatetemple@gmail.com au WhatsApp namba +2349034287285 unaweza pia kumwandikia kupitia Jina la Mtumiaji la Snapchat: drlomi20 atakusaidia nje, asante kwa kusoma,
JibuFutaKwaheri Gerd Ulrich