Jumanne, 24 Januari 2017

MKRISTO AMKA TOKA USINGIZINI VOL..3

πŸ”ΊπŸ”ΊπŸ”ΊπŸ”ΊπŸ”ΊπŸ”ΊπŸ”ΊπŸ”ΊπŸ”ΊπŸ”ΊπŸ”ΊπŸ”ΊπŸ”ΊπŸ”ΊπŸ”ΊπŸ”ΊπŸ”ΊπŸ”ΊπŸ”ΊπŸ”ΊπŸ”ΊπŸ”ΊπŸ”ΊπŸ”ΊπŸ”ΊπŸ”ΊπŸ”ΊπŸ”ΊπŸ”ΊπŸ”ΊπŸ”ΊπŸ”ΊπŸ”ΊπŸ”ΊπŸ”ΊπŸ”ΊπŸ”ΊπŸ”ΊπŸ”ΊπŸ”ΊπŸ”ΊπŸ”ΊπŸ”ΊπŸ”Ί
MKRISTO AMKA TOKA USINGIZINI
 MKRISTO WEWE NI BALOZI WA UFALME WA MBINGUNI HUMU DUNIANI
 Baba Mungu nakushukuru kwaajili ya huyu mpendwa wako anaye fuatilia masomo haya naomba yale yaliyo makusudi yako kwenye hili somo naomba yaweze kutimia juu yake. Tazama umetuweka sisi wanadamu hapa duniani ili tukutumikie wewe na ili tuliheshimu jina lako. pia umetuweka sisi wanadamu hapa Duniani ili kuvitiisha viumbe wote wa kila aina. Ee Mwenyezi Mungu mpe kila asomaye masomo haya uwezo wa kujitambua yeye ni nani na nafasi yake katika kutimiza yaliyo mapenzi yako kwa ulimwengu huu. AMEN
 πŸ”»πŸ”»πŸ”»πŸ”»πŸ”»πŸ”»πŸ”»πŸ”»πŸ”»πŸ”»πŸ”»πŸ”»πŸ”»πŸ”»πŸ”»πŸ”»πŸ”»πŸ”»πŸ”»πŸ”»πŸ”»πŸ”»πŸ”»πŸ”»πŸ”»πŸ”»πŸ”»πŸ”»πŸ”»πŸ”»πŸ”»πŸ”»πŸ”»πŸ”»πŸ”»πŸ”»πŸ”»πŸ”»πŸ”»πŸ”»πŸ”»πŸ”»πŸ”»πŸ”»

Huu ni mwendelezo wa somo letu hili linalomkumbusha Mkristo wajibu wake na nafasi yake katika kutimiza mapenzi ya Mungu kwa ulimwengu huu.
katika mwendelezo huu nitazungumzia kuhusu Mtazamo wa Mungu juu yako ewe mkristo, hasa nafasi yako katika ulimwengu huu.
➤Mkristo ni Balozi wa Ufalme wa Mungu katika Ulimwengu huu.
 Ni hakika kwamba Mkristo ni Balozi wa Ufalme wa Mungu humu duniani. Maana ya balozi ndiyo hii; Balozi ni mwakilishi wa nchi yake katika nchi nyingine ya ugenini. Neno "Balozi" kwa kingereza ni "Ambassador" lenye maana kama hiyo hiyo niliyoitoa ya balozi ambayo inasema 'ambasssdor is a minister of the highest rank sent to a foreign court to represent there his sovereign or country. Sometimes called ambassador-in-residence (http://wikitionary.org). Hivyo tunapozungumza kuhusu Mkristo wewe ni balozi wa Ufalme wa Mungu hapa Duniani tunamaanisha:
➽Mwakilishi wa Ufalme wa Mungu. (Representative of Kingdom of God)
➽ Mtu uliyeaminiwa na Mungu
➽ Mtu uliyepewa uwezo na Mungu wa kuweza kumwakilisha hapa Duniani
➽ Umepewa wajibu na Mungu unapaswa kuutimiza (Mt.10:8)
➽ Mtu mwenye sifa zote na vigezo vyote vya kuwa mfano wa Mungu (Mwa.1:27)
➽ Mungu anakutegemea sana katika kutenda mambo yake hapa Duniani
➽ Muda wako wa kuwepo hapa duniani umehesabiwa (Hutaishi milele katika ulimwengu huu hivyo tumia muda wako vizuri)
➽Wewe sio wa Ulimwengu huu bali ni wa Ufalme wa Mungu (Hivyo ishi ukitambua hapa sio kwenu, kwenu ni mbinguni. Dunia isikufanye ukasahau kwenu) Japo tunaishi ulimwenguni humu kwa namna ya kwimwili lakini una wito ulioitiwa kufanyana kwa muda maalumu, muda ukiisha utatoa hesabu.
➽ Unapaswa kutenda yale ambayo Mungu amekuagiza kuyatenda na sio kutenda mambo ya ulimwengu huu.
➽ Ishi ukitambua kwamba Mungu ndiye atakaye kulipa kwa yale yote utakayo yatenda na sio ulimwengu huu (matendo maovu na matendo mema yote yana malipo yake huko mbinguni. Mungu aliye mwajiri wako amekwisha kukupa)
➽Usitende jambo kwa kuwaangalia wanadamu wanasema nini bali Mungu anasema nini.
➽Tambua kwamba msaada juu ya kila unachokitenda haupatikani popote pale ila kwa Mungu pekee aliyekutuma.(usitafute msaada kwa wanadamu au kwa waganga au kwa miungu mingine)
➽Tambua kwamba mwajiri wako 'MUNGU' amekwisha kuandalia utaratibu mzima wa jinsi utakavyoish; chakula,malazi na makazi pia utaratibu wote wa maisha yako hapa duniani. Ndiyo maana anasema usisumukie kwamba utakula  nini au utakunywa nini.
➽Tambua kwamba unapaswa kuwasiliana na Mwajiri wako kila wakati ili kumfahamisha kila kinachoendelea na njia pekee ya mawasiliano ni 'MAOMBI' 
➽Tambua kwamba kuna mkataba ulioingia wewe na mwajiri wako, unapaswa uufate. 
➽Tambua kuna mambo ambayo mwajiri wako amekwambia uyafuate pindi uwapo humu duniani na unapaswa ufuate (AMRI KUMI)


⧫Ni wakati wa kujitathimini kwamba upo wapi. je! umelala au umeamka? Je! upo kazini kuitenda kazi ya Bwana aliyokuitia hapa ulimwenguni au la? 
⧫Katika  chapisho linalokuja 'VOL....04' Tutaona uchambuzi zaidi wa Mkristo kuwa Balozi wa Mungu hapa ulimwenguni. hii ni sawa na utangulizi tuu wa somo litakalokuja karibu ujiunge nami katika kuliandaa kwa njia ya maombi ili Mungu aliwezeshe likawe na mafanikio makubwa kwa kila atakayesoma.πŸ”œπŸ”œπŸ”œπŸ”œπŸ”œπŸ”œπŸ”œπŸ”œ

⭆Usiache kufuatilia masomo yaliyopita na masomo mbalimbali kwenye blog yangu hii. 
⭆Share kwa wengine nao wapate kusoma na kufaidika kama wewe sasa.
⇲⇲⇲⇲⇲⇲⇲⇲⇲⇲⇲⇲⇲⇲⇲⇲⇲⇲MUNGU AKUBARIKI SANA  ⇲⇲⇲⇲⇲⇲⇲⇲⇲⇲⇲⇲

Mwandishi. Melchizedek Pokeaeli
➧ Unaweza kuyapata masomo mengine sehemu hizi zifuatazo
➢ christiansforum1.blogspot.com
 Facebook: Joyful house in Jesus Christ
WhatsApp https://chat.whatsapp.com/CWsNX9vneY95rYMeuLNW9I
Twitter @johnsonpaulPAUL

Jumatano, 18 Januari 2017

WAKATI WA KUAMKA TOKA USINGIZINI ….Vol.02

πŸ”ΊπŸ”ΊπŸ”ΊπŸ”ΊπŸ”ΊπŸ”ΊπŸ”ΊπŸ”ΊπŸ”ΊπŸ”ΊπŸ”ΊπŸ”ΊπŸ”ΊπŸ”ΊπŸ”ΊπŸ”ΊπŸ”ΊπŸ”ΊπŸ”ΊπŸ”ΊπŸ”ΊπŸ”ΊπŸ”ΊπŸ”ΊπŸ”ΊπŸ”ΊπŸ”ΊπŸ”ΊπŸ”ΊπŸ”ΊπŸ”ΊπŸ”ΊπŸ”ΊπŸ”ΊπŸ”ΊπŸ”ΊπŸ”ΊπŸ”ΊπŸ”ΊπŸ”ΊπŸ”ΊπŸ”ΊπŸ”ΊπŸ”ΊπŸ”ΊπŸ”ΊπŸ”Ί

 WAKATI WA KUAMKA TOKA USINGIZINI ….Vol.02
MKRISTO AMKA USINGIZINI SASA!!!!!
Ahsante Ee Yesu Kristo Kwa NEEMA yako juu ya kila ambaye ni Mkristo anayesoma chapisho hili. Sehemu hii ya pili ya chapisho hili. Ee Baba Mungu mjazie neema ya kudumu katika pendo lako na kuyatenda yale yote yaliyo mapenzi yako. Ni kweli kwamba kuna wengine wengi ambao bado hawajakata shauri la kumpokea Yesu Kristo kuwa Bwana na mwokozi wa maisha yao lakini kupitia wapendwa hawa wachache; maisha yao yakawe mfano kwa wengine yakawe na ushawishi juu ya wengine ili wamkubali Yesu Kristo. Amen!!
πŸ”»πŸ”»πŸ”»πŸ”»πŸ”»πŸ”»πŸ”»πŸ”»πŸ”»πŸ”»πŸ”»πŸ”»πŸ”»πŸ”»πŸ”»πŸ”»πŸ”»πŸ”»πŸ”»πŸ”»πŸ”»πŸ”»πŸ”»πŸ”»πŸ”»πŸ”»πŸ”»πŸ”»πŸ”»πŸ”»πŸ”»πŸ”»πŸ”»πŸ”»πŸ”»πŸ”»πŸ”»πŸ”»πŸ”»πŸ”»πŸ”»πŸ”»πŸ”»πŸ”»πŸ”»πŸ”»πŸ”»

Mpendwa nakusalimu katika Jina la Bwana wetu Yesu Kristo!!!

⭆Utangulizi
Mtu awapo usingizini maana yake ni kwamba hana anachokifanya kwaajili ya maaendeleo yake kimwili, kiakili na kiuchumi hata kiroho. Ndiyo maana Biblia inatuonya kwamba TUSIUPENDE usingizi maana usingizi ni chanzo cha Umaskini.  “Usiache macho yako kupata usingizi, Wala kope za macho ysko kusinzia” Ewe mvivu utalala hata lini? Utaondoka lini katika usingizi wako? Bado kulalala kidogo, Bado kukunja mikono upate usingizi! Hivyo umaskini wako huja kama mnyang’anyi, Na uhitaji wako kama mtu mwenye silaha.” (Mithali 6:4;9-11)
 Usingizi wa Wakristo ni  ubinafsi walionao; kujiona wao pekee ndiyo wanaostahili kuurithi uzima na wengine hawastaili wala hawatakiwi kustahilishwa kupitia Toba. Wakristo wamelala na kujisahau katika ili dimbwi la ubinafsi na kujivuna. Mkristo akimwona Mtua anatenda dhambi basi humsema badala ya kumsaidia hii ni kinyume cha mapenzi ya Mungu. WOKOVU tumeupata bure na kwa neema tu tunapaswa kuutoa bure (Mathayo 10:8) “Pozeni wagonjwa, fufueni wafu, takaseni wenye ukoma, toeni pepo; mmepata bure, toeni bure”.. Ni kusudi la Mungu kwamba ulimwengu wote uokolewe na sio kuangamizwa.
Namshukuru Mungu kwaajili ya Neno lake hili linalowahusu wakristo, Neno linalohusu maisha yao kwaujumla na jinsi wanavyopaswa kuenenda ili wakawe ushuhuda kwa wengine. Katika sehemu ya ya kwanza ya Somo hili tuliona mambo mengi ambayo Mungu anasema nasi na anatukumbusha kwanza ikiwa ni kuhusu Upendo wa Mungu juu ya ulimwengu na huruma yake ambao haukuhesabu makosa yetu bali katika wingi wa maovu yetu yeye alituhurumia na kumtoa mwanaye mpendwa Yesu Kristo ili aje ulimwenguni na kuteswa na kufa kwaajili yetu, pia nilizungumzia kuhusu maisha ya mkristo yanapaswa yamzalie Bwana matunda, matunda hayo ikiwa ni pamoja na kuwafanya wale wasiokoka kuweza kuokoka na hapa utakuwa umempendeza Mungu kwa sababu ndiyo kusudi la Yesu Kristo alipoujia ulimwengu, alikuja kwaajili ya waliopotea awaokoe na kuwatoa kwenye vifungo vya shetani.
Karibu tuendelee na sehemu hii ya pili ya somo hili, japo ni vyema ukasoma na sehemu ya kwanza ya somo hili itakusaidia. 
Wakati wa kuamka usingizini ndiyo sasa mkristo unapaswa kutambua Mungu anafanya kazi pamoja na  wanadamu. Ndiyo maana Neno la Mungu linatuambia kwamba maskani ya Mungu ni pamoja na wanadamu. Kusudi la Mungu juu ya ulimwengu sio kuuhukumu ulimwengu bali ni kuuokoa anatamani katika siku ya mwisho, siku ya hukumu basi asilimia kubwa iwe ni ya wanaoelekea uzima wa milele.  Yesu kristo aliwapa uwezo na mamlaka wale wakristo wa kwanza aliokuwa nao ili wakaiendeleze kazi aliyoianza ya kuhubiri abari njema za ufalme wa mbinguni, na kuwaponya walio wagonjwa na kuwafungua walio kwenye vifungo na kuwasaidia walio katika dhiki (Mathayo 10:1-16). Neno la Mungu linaonyesha nguvu waliopewa wale wanafunzi wa Yesu Kristo juu ya Pepo, na juu ya magonjwa.
     ➻ Mkristo wa sasa Mbona huyatendi haya? Je kuna wagonjwa wangapi katiika eneo ulipo? Je kuna wangapi wanaosumbuliwa na pepo katika eneo ulipo? Umechukua hatua gani ya kupambana na hali hiyo. Je! Uliwaombea au uliwapa msaada wowote? Tambua leo kwamba ile mamlaka Yesu Kristo aliyowapa wanafunzi wake ipo ndani yako wewe umwaminiye Kristo ni wajibu wako kusimama kwa uaminifu katika maombi ili Mungu awezeshe kile alichokipanda ndani yako kifanye kazi. Mathayo 10:8 “Pozeni wagonjwa, fufueni wafu, takaseni wenye ukoma, toeni pepo; mmepata bure, toeni bure”.
    ➻ Unapoitenda kazi ya Mungu kikamilifu basi unautimiza ule mpango wa Mungu ndani yako juu ya ulimwengu na Mungu atakubariki maradufu.  Kusudi la Mungu ni kila goti lipigwe mbele zake na kila ulimi ukiri ya kwamba Mungu ndiye Mfalme juu ya Ulimwengu wote (Ufu.5:13). Ni wajibu wako kutambua sasa unakitu ambacho Mungu anatamani ukifanye popote ulipo kwaajili ya ufalme wa Mbinguni. Mkristo tambua ya kwamba wewe ni balozi wa Ufalme wa Mbinguni hapa Duniani na umepewa mamlaka ya kuyatenda mambo yote katika Jina la Yesu Kristo.

Fuatilia somo mwendelezo wa somo hili kwenye Blog hii hii  http://pokeaeli.blogspot.com au pata masomo mengine mengi kupitia blog hii christiansforum1.blogspot.com
  •        Facebook like page hii Joyful House in Jesus Christ
  •         WhatsApp: 0752513159   

Jumatatu, 16 Januari 2017

NI WAKATI WA KUAMKA TOKA USINGIZINI Vol...01

πŸ”ΊπŸ”ΊπŸ”ΊπŸ”ΊπŸ”ΊπŸ”ΊπŸ”ΊπŸ”ΊπŸ”ΊπŸ”ΊπŸ”ΊπŸ”ΊπŸ”ΊπŸ”ΊπŸ”ΊπŸ”ΊπŸ”ΊπŸ”ΊπŸ”ΊπŸ”ΊπŸ”ΊπŸ”ΊπŸ”ΊπŸ”ΊπŸ”ΊπŸ”ΊπŸ”ΊπŸ”ΊπŸ”ΊπŸ”ΊπŸ”ΊπŸ”ΊπŸ”ΊπŸ”ΊπŸ”ΊπŸ”ΊπŸ”ΊπŸ”ΊπŸ”ΊπŸ”ΊπŸ”ΊπŸ”ΊπŸ”ΊπŸ”Ί
MKRISTO AMKA USINGIZINI SASA!!!!!

⏩⏩⏩⏩Ahsante Ee Yesu Kristo Kwa NEEMA yako juu ya kila ambaye ni Mkristo anayesoma chapisho hili. Ee Baba Mungu mjazie neema ya kudumu katika pendo lako na kuyatenda yale yote yaliyo mapenzi yako. Ni kweli kwamba kuna wengine wengi ambao bado hawajakata shauri la kumpokea Yesu Kristo kuwa Bwana na mwokozi wa maisha yao lakini kupitia wapendwa hawa wachache; maisha yao yakawe mfano kwa wengine yakawe na ushawishi juu ya wengine ili wamkubali Yesu Kristo. Amen.⏪⏪⏪⏪⏪⏪⏪

 ⏬⏬⏬⏬⏬⏬⏬⏬⏬⏬⏬⏬⏬⏬⏬⏬⏬⏬⏬⏬⏬⏬⏬⏬⏬⏬⏬⏬⏬⏬⏬⏬⏬⏬⏬⏬⏬⏬⏬⏬⏬⏬⏬⏬⏬⏬⏬⏬⏬⏬⏬⏬⏬⏬⏬⏬⏬
➤Mpendwa msomaji nakusalimu Katika jina La Bwana wetu Yesu Kristo! 

 Ni hakika kwamba asilimia kubwa ya WAKRISTO katika karne hii ni wakristo kwa kuzaliwa japo kuna wachache ambao ni wakristo kwa kukata shauri walikuwa sio wakristo lakini wamekubali kubatizwa na kuwa Wakristo. na ndio kusudi la Yesu Kristo la kuujia ulimwengu. alifanyika mwili na akakaa kwetu na alikubali kuteswa na kufa kwaajili ya ulimwengu wote ili kila aliyepotea apate wokovu. alisema mwenyewe kwamba amekuja kwaajili ya kile kilichopotea. amekuja kwaaajili ya yule asiyeokoka, hivyo ni furaha kuu mbinguni mwenye dhambi mmoja anapookoka. ni shangwe na furaha tele, pia ni huzuni kwa mwenye dhambi anapofariki. 
➻Ni jukumu lako wewe unayemcha Mungu kuishi maisha yanayompendeza Mungu na yenye mfano kwa wengine. KILA MKRISTO NI MHUBIRI, tuna mhubiri Kristo kupitia matendo yetu. matendo yetu yanamchango wa zaidi ya asilimia 60 katika kkumbadilisha mtu wa imani nyingine. Mf. TUKIISHI MAISHA YA UPENDO- maisha ya upendo ni moja ya maisha ambayo mristo wa aina yeyote ile anapaswa kuyaishi. Ni kweli kwamba majirani aua rafiki yako anaweza kukukosea lakini kumbuka kwamba MUNGU tunaye mwamini na kumtegemea ni PENDO, yeye hakuhesabu maovu yetu tulimkosea sana, tulimkana lakini alituhurumia hata akamtoa mwanaye mpendwa afe kwaajili ya dhambi zetu.
➻Katika sehemu nyengine ya Biblia Yesu Kristo anatuita rafiki zake. Haijalishi ni uovu wa namna gani jirani yako amekutendea lakini unapaswa kumsamehe na kumtendea wema. Neno la Mungu linatuambia kwamba, Jirani yako akikukosea msamehe. lakini linatuambia kwamba mtendee wema jirani yako kwasababu unapofanya hivyo basi unampalia makaa ya mawe juu ya kichwa chake. kumpalia makaa ya mawe juu ya kichwa chake kuna maana hii: unampa uchungu na majuto juu ya kile kitendo ambacho amekutendea.
➻Maisha ya Mkristo yanapaswa yamzalie Mungu matunda. MUNGU hutupa mafanikio na maisha bora ili katika vitu vyote tumzalie matunda. Yohana (sura ya 15) anatuambia kwamba, Yesu Kristo amejiita yeye kama Mzabibu na sisi ni matawi, na kila tawi lisilo zaa basi Mungu ambaye ndiye mkulima basi hulikata. Ili Mungu afurahie maisha yako naakuzidishe katika kila unachokifanya basi unapaswa umzalie matunda. MATUNDA ANAYOHITAJI MUNGU, ni pamoja na wengine wasio mjua Mungu wamjfahamu kupitia wewe; kunena kwako , kutembea kwako hata maamuzi yako.
➻Kwa mali zako na akili pia vyote Mungu alivyokupa unapaswa umtumikie. Yesu Kristo anasema mwenye kanzu mbili umpe asiye nayo. pia mtu mhitaji anapokuja kwako akiwa na uhitaji umkopeshe au umpe basi kama unacho umpe usimwambie aende alafu arudi kesho. zidisha upendo wako kwa kila mmoja lia na anayelia, furahi na anayefurahi huo ndio upendo wa kweli na maisha ya Kikristo. kupitia kufanya hivyo basi utamshawishi yule aliyemtenda dhambi aokoke na kuiacha njia yake mbaya na utapata thawabu mbinguni. 
➻Wewe uliye mhubiri huwezi kumhubiria mtu aache dhambi alafu wewe mwenyewe unatenda. kuwa wakwanza kuchukia uovu na kuuacha kabisa na hapo ata ukimwambia mwenye dhambi aache dhambi basi atakubali. pia msaidie kimwili pia usimwache ateseke hana chakula wakati wewe unacho. msaidie kwa kadri ya uwezo Mungu aliokujalia.  

NB: Mkristo uliozaliwa katika ukristo, jiulize swali hili; kwanini yule asiye mkristo akiokoka anakuwa na bidiii sana ya kumtafuta Mungu na kiwango chake cha imani kinakuwa sana?  

MUNGU AKUBARIKI KWA KUSOMA CHAPISHO HILI!!!!!!!
SHARE CHAPISHO HILI KWA WAKRISTO WENGI UWEZAVYO ILI MKRISTO AAMKE SASA NA KUJITAMBUA.

soma zaidi kwenye ukurasa huu.
christiansforum1.blogspot.com 
pokeaeli.blogspot.com
 facebook. Joyful house in Jesus Christ
WhatsApp: 0752513159